• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wakandarasi Waagizwa Kutimiza Falsafa ya Kazi Iendelee

Posted on: August 5th, 2024


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela amewaagiza wakandarasi watakaotekeleza kazi za ujenzi, ukarabati na matengenezo ya barabara katika Wilaya zote za mkoa wa Geita kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kuhakikisha wanatimiza falsafa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kukamilisha kazi wakati na ubora uliokubalika.

Mhe. Shigela ametoa kauli hiyo tarehe 5/08/2024 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita eneo la Magogo alipokuwa akizungumza na wakandarasi wazawa pamoja na wataalam wa Wakala wa Barabara za vijijini na mijini( TARURA) wakati wa hafla fupi ya utiaji saini wa mikataba kati ya TARURA na Wakandarasi watakaotekeleza shughuli hiyo.


Mkuu wa Mkoa wa Geita ameeleza kuwa mikataba ikamilishwe ndani ya kipindi cha miezi sita ili kumaliza ujenzi kwa wakati kabla ya msimu wa mvua kuanza sambamba na kutiliwa mkazo kwa kipengele cha ubora wa barabara hizo ili wananchi waweze kunufaika na wakandarasi wenyewe kujiwekea rekodi nzuri ya kampuni zao kukumbukwa katika kazi nyingine.

“Napenda kutumia nafasi hii kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa dhamira yake ya kuhakikisha watanzania wote wakiwemo wa Mkoa wa Geita wanapata miundombinu bora ya barabara itakayowarahisishia shughuli zote za usafiri na usafirishaji pamoja na fursa nyingine zitakazopatikana wakati wa matengenezo ya barabara hizo katika maeneo mbalimbali ya mkoa wetu.” Aliongeza Mhe. Shigela.

Meneja wa TARURA Mkoa wa Geita Mhandisi David J. Msechu amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2024/2025 jumla ya shilingi 20,239,286,847.55 kutoka katika vyanzo mbalimbali ikiwemo Mfuko wa barabara( Road fund), Mfuko wa jimbo, Mfuko wa Tozo za Mafuta na Mfuko wa Maendeleo barabara zimeidhinishwa na Serikali kwa ajili ya ujenzi, ukrabati na matengenezo ya barabara katika Mkoa wa Geita.


Mhandisi David Msechu ameongeza kuwa wataalam wote wa TARURA wamejipanga kusimamia kikamilifu na kwa weledi mkubwa utekelezaji wa mikataba hiyo ili kuweza kumalizika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi kuboreshewa huduma za usafiri na usafirishaji, kuwezesha huduma za jamii kama elimu na afya kupatikana kiurahisi, kuongeza ajira kwa wananchi walioko katika maeneo ya kazi na kuinua uchumi pamoja na kuondoa umaskini kwa jamii.

Mikataba 24 yenye jumla ya thamani ya Shilingi Bilioni 9.608 imesainiwa na inategemewa kuanza baada ya siku 14 na itatekelezwa kwa muda wa miezi sita kwenye wilaya zote ndani ya Mkoa wa Geita.





Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa