• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wakurugenzi Geita watakiwa kutenga fedha za Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu

Posted on: March 8th, 2018

Wakurugenzi Geita watakiwa kutenga Fedha za Vikundi vya Akina Mama, Vijana na Walemavu

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya Mkoani Geita kutenga fedha ili kuviwezesha vikundi vya akina mama(Asilimia 4), Vijana(Asilimia 4) na wenye Ulemavu (Asilimia 2) kujikwamua kiuchumi.

Akihutubia wananchi wa Wilaya ya Bukombe katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Mheshimiwa Robert Gabriel amesema kuwa dira ya Serikali ya awamu ya tano iliyo chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ni kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya uchumi wa Viwanda hivyo wanawake wamekuwa na mchango mkubwa katika harakati za kuchochea ukuaji wa uchumi ndani ya nchi kupitia vikundi vya kiuchumi, VICOBA, SACCOS na vikundi vya kijamii. Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa wanawake wamekuwa wakijihusisha na shughuli mbalimbali za kiuchumi kama vile uchakataji wa malighafi ili kuongeza thamani, biashara ndogondogo, ufugaji, ushonaji, kilimo cha mazao na bustani za mboga na matunda ili kujiongezea kipato na kuinua uchumi wa kaya na kutoa mchango katika uchumi wa taifa kupitia sekta isiyo rasmi.

Aidha, amezitaka Halmashauri kuendelea kuchambua na kuvitambua vikundi vya Wanawake na Vijana vyenye mwelekeo wa Viwanda na kuzalisha malighafi kwa ajili ya kulisha viwanda vidogo na vya kati ili vijengewe uwezo kifedha, mafunzo na vifaa ili vichangie azma ya Serikali.

Vile vile Mhandisi Robert Gabriel amesema kuwa ufike wakati jamii ione umuhimu wa kuwalinda Wanawake na Wasichana dhidi ya vitendo vya ukatili kimwili kama vipigo, ubakwaji, ndoa za utotoni na kuwarubuni kimapenzi mabinti wadogo kwa kuwa vitendo hivi vinachangia kwa kiasi kikubwa kukatisha ndoto zao za kujiendeleza kiuchumi, hivyo kurudisha nyuma maendeleo ya kiuchumi katika ngazi ya kaya na taifa.

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kwa Mkoa wa Geita yamefanyika Wilayani Bukombe kwa kauli mbiu ya ''Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Tuimarishe usawa wa jinsia na uwezeshaji wanawake Vijijini''.Ambapo Wanawake wajitokeza kuonyesha bidhaa na shughuli zao mbalimbali.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa