• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wanahabari Wahamasishwa Kuzingatia Sheria ya Huduma za Habari na Takwimu Katika Utoaji wa Taarifa

Posted on: December 10th, 2018

Zaidi ya wanahabari 20 wamepata fursa kushiriki mafunzo kuhusu Utekelezaji wa Mradi wa utoaji huduma za Tohara kinga kwa wanaume kama Afua mojawapo ya kuzuia maambukizi ya VVU katika mkoa wa Geita, mradi wa  miaka mitano kuanzia mwaka (2016-2021),

Hayo yamedhihirika wakati wa mafunzo kwa waandishi wa Habari wa mikoa ya kanda ya ziwa yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Alphendo uliopo Mjini Geita.

Akifungua mafunzo hayo yalioandaliwa na Shirika lisilo la Kiserikali la IntraHealth International Inc,  kwa ufadhili wa Mfuko wa Rais wa Marekani wa kupambana na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) PEPFAR kupitia CDC, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Geita, Dkt. Japhet Simeo amewataka waandishi kusaidia ufikishaji wa taarifa sahihi kwa wananchi na kwa wakati.

“Tunaamini kuwa nyie ni chachu ya kufikisha taarifa, lakini leo tumewaita hapa lengo kuu ikiwa ni kuhakikisha mnatusaidia kufikisha habari hii mahali ambapo hatufiki, mkizifikisha kwa usahihi na tutawapitisha kujua hali halisi ya maambukizi na mjue mbinu gani tunazotumia” amesema Dkt. Simeo.

Dkt. Simeo ameendelea kusema kuwa, wanahabari ni muhimu kukumbuka juu ya sheria zilizopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sheria ya Huduma za Habari na ya Takwimu ambapo ni wajibu wa kila mtoa habari au taarifa kutoa takwimu zilizo sahihi, sizizowachanganya wananchi, zinazochochea maendeleo na si migogoro huku wananchi wakipata haki yao ya kupata taarifa, 

Vilevile ameeleza changamoto ya kutoweza kuwabakisha wananchi waliogundulika kuwa na maambukizi ya UKIMWI ili waendelee kupata dawa za kufubaza maambukizi hayo kutokana na aina ya shughuli za kiuchumi wanazojiusisha nazo mkoani Geita kama vile ufugaji, uvuvi na uchimbaji madini, shughuli zinazosababisha uhamaji wa wananchi hawa.

Aidha Dkt. Simeo alieleza kuwa zipo jitihada kuhakikisha maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI yanapungua kutokana na ongezeko lililopo kwa sasa kutoka asilimia 4.7% hadi 5% ambalo limetokana na uwepo kampeni zinazoendelea kufanyika juu ya tohara huku ikihakikishwa wote wanaofanyiwa tohara wanapimwa na VVU.

Akitambulisha Shirika la IntraHealth International Inc, Dkt. Peter Sewa ambaye ni Mshauri Huduma za Tohara Mkoa wa Geita alisema  wanatarajia kuanza kufanya tohara kwa watoto wachanga wenye umri kuanzia mwaka 0 hadi miezi 2 kwa mwaka 2019

Naye Mkufunzi wa mafunzo hayo Bw. Temigunga Mahondo amewataka waandishi kuzingatia weledi katika uhabarishaji wa sekta ya afya wakitambua kuwa wao ni wafikisha taarifa kwa jamii na kwamba endapo watapotosha wataharibu sifa yao binafsi lakini pia jina la chombo wanachokitumikia.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa