• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wananchi Geita Kunufaika na Huduma ya Maji

Posted on: May 31st, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Senyamule amewataka wananchi wa mkoa huo kuwa na utaratibu wa kutunza vyanzo vya maji ambavyo vimekuwa ni muhimu kwao.

Ameyasema hayo leo Mei 31, 2022 wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya utekelezaji mradi wa kuboresha huduma ya maji mjini Geita unaotekelezwa na serikali kupitia Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Geita (GEUWASA).

"naipongeza GEUWASA kwa kazi kubwa wanayoifanya, jambo hili limenilidhisha kuona mradi huo unakamilika hata kabla ya wakati uliopangwa" amesema Mh. Senyamule

Amesema pia wananchi zaidi ya 6,250 watanufaika na mradi huu, hivyo ameutaka Uongozi kuhakikisha kukamilika kwa mradi huo kama yalivyo maelekezo ya serikali ili wananchi wapate huduma kwa wakati.


Ikiwa zimebakia siku 30 kufikia tarehe ya mwisho ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na fedha za Mpango wa Maendeleo na Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO-19, Mh. Senyamule alisema,

 “tunamshukuru Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwakuwa yeye alikuwa na utashi wa kupambana na janga la UVIKO kwa kuamua kutoa fedha hizo kujenga miradi mbalimbali ikiwemo huu wa maji ambao utachangia ongezeko la 4% na kuufanya mji wa Geita kupata maji kwa 75% kutoka 71% ya awali na kuwezesha wananchi takribani 6,250 kupata huduma ya maji. Vilevile, niwapongeze GEUWASA kwa utekelezaji unaozingatia muda na hivyo niagize na taasisi nyingine zenye ujenzi wa miundombinu kwa fedha za mapambano dhidi ya UVIKO-19 kukamilisha miradi hiyo mapema iwezekanavyo”.


Mhe.Senyamule aliongeza kuwa, ni vyema GEUWASA kuhakikisha wanapanda miti rafiki kwa mazingira ili kuendelea kutunza vyanzo vya maji lakini pia kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili wasiharibu vyanzo hivyo na kutoa wito kwa wananchi kutumia vizuri rasiliamali maji na kuwa walinzi wa miundombinu kwa kutoa taarifa kwa mamlaka juu ya uharibifu au wizi wa miundombinu hiyo.

Awali akisoma taarifa ya utekelezaji mradi, mhandisi Isaac Mgeni alisema, mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya Tshs.511,906,928.22, unalenga kuwahudumia wananchi wa Ishinde, Igembesabho, Fadhili Bucha, Mwabasabi, Kasamwa, Kanyala na Buhalahala pale utakapokamilika kwakuwa hadi sasa upo kwenye 98% ya utekelezaji na kwamba hadi sasa, jumla ya wateja wapya 123 wa maeneo ya Kasamwa na Buhalahala wamekwisha unganishiwa huduma hiyo.

Naye Ndg.Nestory Madaha kwaniaba ya Mfawidhi wa Kituo cha Afya Kasamwa kinachohudumia takribani wateja 1,500-2,000 alisema, “tunaishukuru sana serikali yetu pendwa kwa kutueletea huduma ya maji ambapo awali tulitumia fedha nyingi kununua maji na kwa hatua hii, kituo chetu kitaendelea kuwa kisafi, wagonjwa wanapata huduma nzuri na tutaepuka magonjwa yatikanayo na uchafu”



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara Wadogo Wahamasishwa Kujisajili

    May 15, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa