• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wananchi Geita Wahamasishwa Kutumia Nishati Mbadala

Posted on: September 7th, 2025


Wananchi waishio katika mkoa wa Geita wamehamasishwa kutumia nishati mbadala ya gesi katika kupikia pamoja na mkaa mbadala ili kutimiza agizo la Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linalosisitiza matumizi ya nishati safi na salama ili kupunguza uharibifu wa mazingira.

Hamasa hiyo imetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge kitaifa 2025 Ndugu. Ismail Ali Ussi kwa nyakati tofauti katika Halmashauri Zote za Mkoa wa Geita wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ulioanza mbio zake ndani ya Mkoa huo kuanzia tarehe 01 hadi 06 Septemba 2025.

Ndg. Ismail Ali Ussi ameeleza kuwa maeneo mengi ya Nchi yetu yamekumbwa na janga la uharibifu wa mazingira hususan ukataji miti kwa lengo la kuchoma mkaa na kupata kuni za kupikia majumbani, hali ambayo inahatarisha uendelevu wa uoto wa asili na athari nyingine zinazotokana na ukataji miti hovyo, Hivyo wananchi wote mnatakiwa kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na kutumia nishati ya gesi.

Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Ndg. Philip Makungu amesema kuwa wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, Halmashauri yake imegawa mitungi 100 kwa makundi maalum ambapo mitungi 50 imegawiwa kwa mama lishe katika Kata ya Makurugusi na mitungi 50 katika Kata ya Chato na Muungano. Pia mitungi 400 itauzwa na Wakala wa Nishati Vijijini( REA) kwa bei ya punguzo ili kuwezesha wananchi wa hali mbalimbali kumudu gharama hiyo.

Ndg. Philip Makungu ameongeza kuwa sambamba na zoezi la ugawaji wa mitungi ya gesi Wilaya imeendelea kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi na bora hasa gesi, umeme na majiko banifu ya kupikia katika maeneo ya wachimbaji wadogo, shule na vyuo vilivyoko wilayani Chato. Pia wanaendelea kushirikiana na REA kuuza mitungi kwa bei ya punguzo pamoja na kuhimiza Taasisi zenye watu Zaidi ya 100 kutumia nishati safi katika kupikia.

“Kupitia kampeni ya matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia, manufaa mbalimbali yamefikiwa ikiwa ni pamoja na Taasisi mbalimbali kuanza kutumia mfumo wa nishati safi na salama, Kuwafikia wachimbaji madini 126 na kuwahamasisha kutumia umeme wa petrol au dizeli katika kutoa maji kwenye mashimo pamoja na kutoa elimu katika shule 10 za Sekondari ili kutunza mazingira na bionuai kwa vizazi vya sasa na vya baadae.” Aliongeza Ndg. Philip Makungu.

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 zimeongozwa na kauli mbiu isemayo “Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu.”











Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Geita Wahamasishwa Kutumia Nishati Mbadala

    September 07, 2025
  • TFS Wapongezwa na Mwenge wa Uhuru 2025

    September 06, 2025
  • Vijana Wakumbushwa Kuchangamkia Mikopo ya Halmashauri

    September 03, 2025
  • Wawekezaji Wahamasishwa Kuwekeza Miradi ya Kijamii

    September 04, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa