• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wanawake Wahamasishwa Kujiunga na Majukwaa ya Kiuchumi

Posted on: August 22nd, 2024


Wanawake waishio katika Halmashauri zote za Mkoa wa Geita wamesisitizwa kuhakikisha wanajiunga na majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi kuanzia ngazi ya vijiji na mitaa ili waweze kutambulika na kuunganishwa kwenye fursa mbalimbali zinazopatikana ambazo zitawawezesha kujikwamua kimaisha wao binafsi pamoja na familia zao.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na makundi maalum Ndg. Felister Mdemu alipofanya ziara ya kikazi katika Halmashauri za Mji Geita, Wilaya ya Geita na Bukombe kwa lengo la kuzungumza na makundi ya wanawake yanayoratibiwa na Wizara yake pamoja na kukagua shughuli zao wanazozifanya.

Ndg. Felister Mdemu ametoa pongezi kwa Mkoa wa Geita kwa kufikisha wanachama 11765 ambao wameshajiunga na Jukwaa la Uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi katika Halmashauri zote za mkoa wa Geita kwa lengo la kuwawezesha wanawake hao kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo katika maeneo yao.


“Napenda nitumie fursa hii kuwapongeza Maafisa Maendeleo ya Jamii wote wa Mkoa wa Geita kwa namna mnavyofanya kazi kwa bidii na kwa ushirikiano mkubwa, hakika jitihada zenu zimejidhihirisha. Pia natoa wito kwa jamii, Taasisi za Serikali na watu binafsi katika Mkoa wa Geita kuunga mkono juhudi za wanawake kwa kununua bidhaa wanazozalisha kwa wingi hususan wakati wa sherehe na matukio mbalimbali ambapo bidhaa hizo zitahitajika.” Aliongeza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii.

Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya jinsia katika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Bi. Juliana Kibonde ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe kwa kuanzisha vikundi 12 ambavyo vimezaliwa kutoka katika Umoja wa Wanawake Wachimbaji Bukombe na kushauri Halmashauri nyingine za Mkoa wa Geita kuiga mfano huo ili wanawake wengi Zaidi waliopo kwenye jamii waweze kujiunga na vikundi ili wawezeshwe kiuchumi na kukataa kabisa ukatili wa kijinsia.

Mwenyekiti wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi Mkoa wa Geita Bi. Wancy Siwale ameeleza baadhi ya mafanikio yaliyofikiwa na jukwaa hilo ni pamoja na kuanzisha SACCOS, kushiriki katika shughuli mbalimbali za jukwaa kitaifa kama Kampeni ya 27 ya kijani pamoja na kuendelea kushirikiana na Taasisi za Serikali, binafsi na wadau wengine wa maendeleo katika jitihada za kuwakwamua wanawake kiuchumi.


Uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi kupitia mikopo ya asilimia 10 na uwepo wa majukwaa ya uwezeshaji wanawake kiuchumi ni utekelezaji wa progamu ya kitaifa ya Jukwaa la kizazi chenye usawa ambalo Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kinara katika utekelezaji wa eneo namba 2 la Haki na Usawa kiuchumi.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa