• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wanawake Watajwa Kama Sehemu ya Hamasa, Toharakinga kwa Wanaume Geita

Posted on: December 13th, 2018

Ikiwa zimesalia siku chache kabla ya kumalizika kwa robo ya kwanza, ya Kampeni ya Toharakinga kwa Wanaume wenye umri kuanzia miaka kumi na kuendelea inayoendeshwa mkoani Geita, kundi la wanawake limebainika kuwa chachu ya kufanikisha mpango huo kutokana na wengi wao kuwahimiza wanaume wao na watoto kwenda kufanyiwa Tohara.

Hadi kufikia Sepetemba 2018, wanaume 115, 000 kati ya 119, 000 waliolengwa kufanyiwa tohara Mkoani Geita walikuwa wamefikiwa na kuhudumiwa katika kampeni inayoendeshwa na Serikali kwa ushirikiano na Shirika lisilo la kiserikali la IntraHealth International kwa ufadhili wa Mfuko wa Rais wa Marekani wa Kupambana na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) PEPFAR kupitia CDC,

Kituo cha Afya Katoro ni kati ya vituo 23 vya muda na 13 vya kudumu vinavyotoa huduma hiyo ambayo kabla ya kutolewa wanaume wanaofika kufanyiwa tohara hupitia hatua kadhaa ikiwemo kuandikishwa, kuelimishwa na kupimwa virusi vya UKIMWI kabla ya huduma.

Msimamizi wa Kituo hicho, Bw. Faustine Edward alisema muitikio wa wananchi umekuwa mkubwa kiasi cha kuwafanyia tohara wanaume kati ya 10 hadi 30 kwa siku.

“Mwitikio ni mkubwa sana, wateja ni wengi, hadi tunafikiria kuongezewa muda kwakuwa tulianza zoezi hili mwezi Novemba 15, 2018 na mwisho ni mwezi Desemba 15, 2018; Lakini pia niwapongeze akinamama, wamekuwa mabalozi wazuri kwa kuwaleta watoto wao lakini pia kuwashawishi waume zao kuja kufanya Toharakinga salama hadi kutuwezesha kupata watu 10 hadi 30 kwa siku,” alisema Bw. Edward

Pamoja na muitikio huo, Bw. Edward Alisema zipo baadhi ya changamoto zinazoikabili kampeni hiyo ikiwemo upungufu wa miundombinu ya jengo la kutolea huduma kwa sasa, imani potofu kutoka kwa baadhi ya wananchi kuhusu tohara na kutozingatia ushauri wa kitaalam kwa baadhi ya wanaofanyiwa tohara kutumia njia za asili za kutibu vidonda.

“Baadhi ya wanaotahiriwa wakirejea majumbani husikiliza na kutumia ushauri wa mitaani ikiwemo kutumia kinyesi cha Ng’ombe kupakwa kwenye kidonda wakiamini husadia kupona haraka, jambo linalosababisha madhara kiafya. Tunakabiliana na tatizo hili kwa kutoa elimu kwa wananchi na tiba sahihi tatizo linapojitokeza,”alisema Edward

Kwa upande wake Bi. Winfrida John, Mkazi wa Ludete Stooni amekuwa shuhuda wa kupitia mtoto wake kutosumbuliwa na maambukizi kwenye njia ya mkojo (UTI) baada kufanyiwa Toharakinga aliyosema inasaidia usafi na kuepusha magonjwa mbalimbali ya zinaa huku akiwaasa wanawake na wananchi kwa ujumla kujitokeza kuunga mkono kampeni hiyo.

Bw. Masunga Maduhu ni mmoja wa wanaume waliofanyiwa Toharakinga wakiwa na umri wa miaka 34, ambaye katika mahojiano alisema hakupata madhara wala kusikia maumivu wakati wa tohara na kuiomba Serikali na wadau wengine kuendeleza huduma hiyo hadi maeneo ya vijijini.

“Pamoja na faida ya kujiepusha na maambukizi ya UKIMWI kwa asilimia 60, tohara pia imeniongezea kujiamini kiasi cha kuweza kujisaidia haja ndogo bila hofu mbele ya watu wengine kulinganisha na awali nilipokuwa naona aibu nikijificha kwa sababu nilikuwa sijafanyiwa tohara,” alisema Maduhu

Naye Bw. Peter Ngaseba, Mkazi wa Katoro Stooni amesema, usafi na kuepuka maambukizi ya virusi vya UKIMWI kupitia hamasa inayoendelea kufanywa na wataalam mtaani wakiwapa elimu na vipeperushi ndiyo imempa msukumo.

Alienda mbali zaidi kwa kusema tohara imeongeza hamasa na uwezo wake katika tendo la ndoa kutokana na kujiamini.

Vilevile, tunatakiwa kuelewa kwamba Toharakinga salama inazo faida kemkem zikiwemo kupunguza uwezekano wa kupata magonjwa ya zinaa ambayo nayo huchangia kwa kiasi kikubwa maambukizi ya virusi vya UKIMWI, kupunguza uwezekano wa kupata saratani ya kichwa cha Uume, saratani ya mlango wa kizazi kwa akina mama, kukosa uwezo wa kutungisha mimba, uvimbe wa kichwa cha Uume na magonjwa mengine ya zinaa.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa