• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wawekezaji Wahamasishwa Kuwekeza Miradi ya Kijamii

Posted on: September 4th, 2025


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 Ndugu. Ismail Ali Ussi ametoa hamasa kwa wawekezaji wa ndani kutumia vyema fursa zilizowekwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwekeza katika miradi ya sekta mbalimbali za kijamii ikiwemo shule, hospitali na nyinginezo.

Ndg. Ismail Ali Ussi ametoa kauli hiyo tarehe 4 Septemba 2025  alipokuwa akizungumza na hadhira iliyojitokeza kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi katika Kituo cha Afya Gakala kilichopo Wilayani Mbogwe na kinamilikiwa na mwekezaji mzalendo.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 ameeleza namna alivyofarijika kuona dhana ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya watanzania wenyewe kuijenga Nchi yao inatekelezwa na wawekezaji wachache wanaojitoa kuwekeza katika miradi inayotoa huduma za kijamii na kuongeza ajira za wananchi wa maeneo husika ambao wameajiriwa katika miradi inayoanzishwa na wawekezaji.

“Mwenge wa Uhuru umewaheshimisha wananchi wa Mbogwe kupitia mradi huu mkubwa na sasa huduma za afya katika Wilaya ya Mbogwe zimezidi kuboreshwa baada ya mwekezaji mzalendo mwenye tija ya kuijenga Nchi yake ameamua kuonyesha kwa vitendo kwa kuwekeza kwenye sekta ya afya badala ya miradi mingine yenye mlengo wa kujiingizia kipato binafsi kikubwa.” Aliongeza Ndg. Ismail Ali Ussi.


Ndg. Ismail Ali Ussi ameongeza kuwa mwekezaji huyo ameondoa hofu kwa wananchi na Serikali kwa ujumla katika upatikanaji wa huduma zote katika Kituo cha Afya Gakala ikiwemo huduma ya kujifungua ambayo ni muhimu sana katika utatuzi wa changamoto ya vifo visivyotarajiwa vya kina mama na watoto wachanga kutokana na kukosekana kwa huduma hiyo muhimu kwa haraka na karibu na makazi yao.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Afya Gakala Ndg. Bunga Dadu amesema kuwa lengo la ujenzi huo ni kusaidia wananchi wa Kata ya Bukandwe na kata jirani kupata huduma bora za afya za kibingwa jirani na makazi yao.

  Ndg. Bunga Dadu ameeleza kuwa ujenzi wa Kituo hicho wenye thamani ya shilingi Bilioni tatu ulianza rasmi mwezi Disemba mwaka 2024 kwa hatua ya kwanza ya ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje( OPD), jengo la mama, baba na mtoto, jengo la utawala, nyumba ya watumishi, jengo la upasuaji, kichomea taka na shimo la kutupia kondo la nyuma.

Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wananchi Geita Wahamasishwa Kutumia Nishati Mbadala

    September 07, 2025
  • TFS Wapongezwa na Mwenge wa Uhuru 2025

    September 06, 2025
  • Vijana Wakumbushwa Kuchangamkia Mikopo ya Halmashauri

    September 03, 2025
  • Wawekezaji Wahamasishwa Kuwekeza Miradi ya Kijamii

    September 04, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa