• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Zaidi ya Milioni 293 za RUWASA Zawatua Ndoo Kichwani Wananchi 10,448 Nzera&Bugando

Posted on: March 19th, 2023

Na Boazi Mazigo-Geita

Mkuu wa mkoa Geita Mhe.Martine Shigela amezindua mradi wa maji utakaowahudumia wananchi 10,448 katika Vijiji vya Nzera na Bugando, kata ya Nzera, Tarafa ya Bugango, Jimbo la Geita ndani ya halmashauri ya wilaya Geita, huku akiwapongeza wananchi wa kata hiyo kuzindua mradi huo wakati nchi ikielezea mafanikio ya serikali ya awamu ya sita kwa kipindi cha miaka miwili chini ya uongozi wa Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuwasihi kutunza miundombinu lakini pia kuhakikisha wanaunganisha maji hadi nyumbani.

Mhe.Shigela ameyasema hayo Machi 19, 2023 katika eneo la soko la Nzera akizungumza na wananchi baada ya kutembelea na kupanda mti aina ya Mdodoma kwenye chanzo cha maji kwenye mradi huo katika kitongoji cha Lukelege unaotekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ambapo amewasihi kamati za maji wasigeuze mradi huo shamba la bibi.

“niwapongeze kuchagua kuzindua mradi siku ambayo mhe.Rais wetu Dkt.Samia Suluhu Hassan anatimiza miaka miwili madarakani, huu ni mradi kielelezo. Pia niwapongeze RUWASA kwa kazi nzuri lakini kubwa zaidi niwaombe wakazi wa Nzera tujiandae, Nzera inakuwa mji hivyo tukubali kupangwa na tuwe tayari kuchangamkia fursa baada ya ukamilishwaji wa bandari ya Nkome itakayojengwa hivi karibuni, lakini pia uwepo wa reli ya kisasa SGR pamoja na daraja la Magufuli (Kigongo-Busisi)”, alisema Mhe.Shigela

Mwisho, Mhe.Shigela alimaliza kwa kuwasisitiza wazazi kuwapeleka watoto shule wapate elimu ili kuwa na wataalam wa hapo baadaye, vilevile amewaalika kutumia huduma za afya za kibingwa zinazotolewa na Hospitali ya Rufaa ya Kanda Chato yenye vifaa vya kisasa kama CT-Scan, MRI, Dialysis Machine n.k pamoja na kuagiza wataalam ambao wana kero ambazo hawajazitatua kwa wananchi wafanye hivyo haraka kabla hajarudi kufanya ziara kujionea ujenzi wa barabara Km 20 kiwango cha lami katika kipande cha kwanza kutoka Nkome-Sungusila.

Naye mbunge wa jimbo la Geita Mhe.Joseph Kasheku Msukuma alisema, anaipongeza sana RUWASA na kwamba katika jimbo hilo miradi mingi ya RUWASA inaendelea kutekelezwa hivyo kutumia fursa hiyo kuyasema mafanikio ya serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan akiwasihi wananchi kuchangia huduma ya maji kwa kujisajili ili waunganishiwe maji huku akiwataka wananchi anaowaongoza kuyapa mkono maendeleo na si kuyapinga.

Akisoma taarifa ya mradi Meneja wa RUWASA Wilaya Geita Mhandisi Sande Batakanwa alisema, mradi huo wa kisima kirefu una kina cha Mita 50 chenye uwezo wa kuzalisha lita 3,600 za maji kwa saa pamoja na mtandao wa bomba wenye urefu wa Km. 6.679 na ujenzi wa vituo 10 vya kuchotea maji. Mradi ulianza kutekelezwa Desemba 2021 na ulikamilika Desemba 2022 na utahudumia wananchi zaidi ya 10,448 kwa gharama ya shilingi milioni mia mbili tisini na tatu na elfu hamsini na mia tano na nane na senti hamsini na nane (293,050,508.58) kutoka katika chanzo cha Mapambano dhidi ya UVIKO-19

Mhandisi Batakanwa aliongeza kuwa, ukamilikaji wa mradi huo unapunguza muda uliokuwa unatumiwa na wananchi kufuata maji umbali mrefu ambapo kwa sasa muda huo utatumika kwenye kujenga uchumi. Vilevile, utapunguza magonjwa yatokanayo na ukosefu wa maji safi na salama kama vile kuhara, homa ya matumbo na kipindupindu, lakini kubwa zaidi kufungua fursa za kiuchumi kama uendeshaji viwanda vidogo na bustani za mbogamboga.  

Sherehe hizo za uzinduzi zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali ikiwemo kamati ya usalama mkoa, viongozi wa CCM Wilaya na Kata pamoja na watumishi wa RUWASA Mkoa na Wilaya.

Geita, Hakuna Kilichosimama



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa