• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Zaidi ya Vijana Zaidi ya 12,000 Kujikwamua Kiuchumi Kupitia EACOP

Posted on: August 19th, 2025


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Doto Biteko amezindua rasmi mradi wa kuwawezesha vijana kujikwamua kiuchumi katika maeneo yaliyopitiwa na Bomba la mafuta Ghafi la Afrika Mashariki unaotarajiwa kuwanufaisha Zaidi ya vijana elfu 12.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi huo iliyofanyika katika Uwanja wa kijiji cha Bukombe Wilayani Bukombe Geita tarehe 18 Septemba 2025 Mhe. Dkt. Doto Biteko ameeleza kuwa lengo la mradi huo ni kuwawezesha vijana kiuchumi kupitia fursa mbalimbali zitokanazo na Bomba la mafuta ghafi katika mikoa ya Geita, Kagera, Tabora na Tanga kwa awamu ya kwanza.

Dkt Biteko amesema mradi huo ni sehemu ya kuongeza mnyororo wa thamani katika mradi wa EACOP ambapo juhudi zote hizi ni kuhakikisha mradi unaleta manufaa kwa jamii na kusaidia kupunguza umasikini wa watu na kuwaasa vijana waliopata fursa kwenye mradi wa EACOP kulinda raslimali za kampuni na kuwajibika kwa matakwa ya mkataba ili wawe mabalozi wa watanzania.

Dkt. Biteko ameongeza kuwa hadi Julai 2025, serikali imewekeza takribani sh Trillioni 1.125 na kusaidia mradi kutoa ajira 9,194 za moja kwa moja ikiwemo vijana 170 waliofadhiliwa masomo ya ujuzi na ufundi stadi na kisha kuajiriwa. Kadhalika kampuni imetoa ufadhili wa vijana 238 kwa ajili ya kwenda kusoma kwenye vituo mbalimbali nchini, haya yote ni manufaa ya mradi huu tunaouzungumza hapa.


Meneja Uwajibikaji na Uwekezaji kwa Jamii wa EACOP Bi. Clare Haule amesema programu ya uwezeshaji vijana kiuchumi inazingatia fursa kwa vijana, huduma za maji, afya na usalama wa jamii, nishati endelevu na mazingira na kueleza kuwa katika awamu ya kwanza ya program ya uwezeshaji vijana itanufaisha mikoa minne ambayo ni Geita, Kagera, Tabora na Tanga kati ya mikoa nane inayopitiwa na mradi wa EACOP.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EACOP, Geofrey Mponda amesema hadi kufikia mwishoni mwa robo ya mwaka 2025 zaidi ya asilimia 80 ya ajira katika mradi zimejazwa na wazawa kutoka Tanzania na Uganda.

Ndg. Mponda amefafanua kuwa serikali imetoa muongozo kuhakikisha mpango wa ajira za kigeni inaendana na makubaliano ya wanahisa na watanzania wanapewa kipaumbele katika nafasi za kazi zinazohitajika na kampuni ya EACOP na kueleza kuwa mwaka 2024 EACOP ilianzisha mafunzo maalum na kuweza kudahili watanzania vijana 112 na waganda 29 walipata fursa ya kufanya mafunzo ya nadharia na vitendo na baada ya kuhitimu wataajiriwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ameeleza kuwa Serikali ya Mkoa wa Geita itaendelea kushirikiana na wataalam wanaofanya kazi katika mradi wa Bomba la mafuta na kueleza  baadhi ya  faida zinazopatikana kupitia mradi huo ni pamoja na wananchi kunufaika na mnyororo wa thamani kwa kufanya biashara mbalimbali pamoja na ajira za muda mfupi na mrefu kwa jamii .

Tangu kuanza ujenzi wa mradi wa Bomba la mafuta ghafi Afrika Mashariki jumla ya kampuni 200 za kitanzania zimepata zabuni katika mradi huo ambao umefikia asilimia 65 ya utekelezaji.

Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Zaidi ya Vijana Zaidi ya 12,000 Kujikwamua Kiuchumi Kupitia EACOP

    August 19, 2025
  • GESECO Kinara Mtihani wa Mock Kidato cha NNne Kanda ya Ziwa

    August 19, 2025
  • Serikali Yatoa Zaidi ya Bilioni 40 Kujenga Miundombinu ya Umwagiliaji Geita& Mwanza

    August 12, 2025
  • UZINDUZI WA DAWATI LA HUDUMA ZA USTAWI WA JAMII KATIKA MANISPAA YA GEITA

    August 07, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa